Posts

Showing posts from May, 2014

WAKATI WANAFUNZI WA VYUO VIKUU TANZANIA WAKILIA BOOM,KENYA KWACHAFUKA,WANAFUNZI WAFANYA MAPAMBANO NA ASKARI KISA ONGEZEKO LA ADA

Image
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Kenya wamezua vurugu wakipinga mpango wa serikali kutaka kuongeza karo katika vyuo vikuu vyote vya umma. Polisi walipambana na wanafunzi hao kwa kutumia gesi ya kutoa machozi kutawanya wanafunzi hao ambao walizua vurugu mjini na kuwapora abiria huku wakiharibu magari ya umma na yale ya abiria katika barabara kuu ya Uhuru katikakati ya jiji la Nairobi. Pia waliripotiwa kuvunja maduka na kuharibu mali ya watu. Wachuuzi walilazimika kuondoka mjini huku polisi wakipambana na wanafunzi hao ambao waliungana kutoka vyuo vikuu mbali mbali kote nchini Kenya. Awali maandamano yao yalikuwa salama ingawa baadaye wanafunzi hao walioanza kuandamana tangu saa nne asubuhi walianza kuzua rabsha na kulazimisha polisi kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya. Wanafunzi hao wanaandamana kupinga mapendekezo ya serikali kuongeza karo ya vyo vikuu , ingawa waziri wa elimu ya juu Profesa Jacob Kaimenyi amesema kuwa serikali bado haijatoa tamko r...

DAKTARI ASAHAU KITAMBAA TUMBONI MWA MAMA MJAMZITO WAKATI WA UPASUAJI

Image
  Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr Seif Rashid.  MKAZI wa wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Mwamini Adamu ametolewa mfuko wa kizazi na kukatwa sehemu ya utumbo baada ya mganga wa idara ya upasuaji katika wilaya hiyo kusahau kitambaa tumboni kwa mwanamama huyo wakati akijifungua.  Kutokana na kumsababishia ulemavu huo kwa uzembe, Mwamini ameifikisha Halmashauri ya wilaya ya Urambo kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Magharibi akidai fidia ya Sh milioni 500. Mwamini ambaye anadai kuwa alipwe kiasi hicho cha fedha kutokana na uzembe wa uliofanywa na Dk Jacob Kamanda aliyemfanyia upasuaji wakati wa kujifungua na kumsababishia aondolewe mfuko wa kizazi pamoja na kukatwa utumbo. Mwamini pamoja na mumewe Idrisa Jafari katika madai yao wametaka walipwe fedha hizo kutokana na makosa ya uzembe uliofanywa na wataalamu wa upasuaji kwa kuacha kitambaa tumboni mwa mama huyo. Akitoa ushahidi wake mbele ya Jaji Amir Mruma jana, mama huyo alidai kuwa Januari 6 mwaka 2011 alijifungua kwa upasu...

RAIS KIKWETE AKUBALI KUFUTWA KODI YA LAINI ZA SIMU, ASAINI HATI YA DHARURA KUFANYIWA MAREKEBISHO MUSWADA WA FEDHA WA 2013

Image
By Butije Hamisi- Dar es Salam Rais wa  jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete amesaini hati ya dharura (Certificate of Urgency)  kufuta kodi ya Tsh. 1000 kwa mwezi kwa kila laini ya simu iliyopitishwa na Bunge na kuwekwa kwenye bajeti ya 2013/2014. Kufuatia hatua hiyo Bunge limepelekewa taarifa hiyo na kulichukua kama dharura ili Muswada wa Fedha wa Mwaka 2013 ufanyiwe marekebisho ya kuondoa tozo ya kodi kwa kadi za simu.. Bunge la Bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2012/13 lilipitisha kodi ya Sh1,000 kwa kila kadi ya simu, hatua ambayo ilipingwa na wabunge wengi. Akithibitisha utiaji saini huo Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba alisema jana kuwa Rais Kikwete alitia saini hati hiyo juma hili. “Muheshimiwa Rais ametia saini hati ya dharura kufanyika marekebisho kwa muswada wa fedha wa mwaka 2013 kuondoa tozo ya kodi kwa laini za simu” alisema Makamba Makamba alisema suala la muswada huo kurudishwa bungeni l...