Posts

Showing posts from February, 2012

MAKATAZO YA KISHARI`AH KWA WANAWAKE

Imekusanywa Na: Abu Faatwimah     Katazo La Kutokuwa Na Shukurani [Kukanusha] Ihsaan Huu dada yangu Muislamu ni uwanja mwingine wenye hatari kubwa, na kwa bahati mbaya ni kuwa wengi miongoni mwa wanawake kwa masikitiko makubwa wameuingia na kuamua kuwa ni katika sehemu zao za kuishi na kutafuta kuridhiwa au kupewa ruhusa ya kwenda watakapo hata kama ni kwenye maasi na pasipo mridhia Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) . Wanawake wengi siku hizi wanapotaka jambo ambalo wanaelewa kuwa mume hatoridhika nalo au halipendi au hata wakati mwingine hayuko tayari nalo kwa sababu moja au nyingine au hata kama hataki ni haki yake; huwa silaha yao kubwa ya kutaka wakubaliwe walitakako kusema usemi wao mashuhuri na wenye kupendeza katika midomo yao: Sikupata kuiona kheri hata siku moja kutokana nawe; yote kwa kuwa amekataliwa siku hiyo alitakalo au amezuiliwa kufanya alitakalo au kwenda atakapo. Mke ni mwepesi wa kusahau au kujisahaul...

SIKUKUU YA WAPENDANAO NA HUKUMU YAKE

Image
BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu was Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa ‘Aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa Ba’ad, Allaah سبحانه وتعالى Ametuchagulia dini ya Kiislamu ambayo ndio dini ya haki na Hatokubali dini yoyote nyingine kama Anavyosema: ((وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الإِسْلاَمِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ))   ((Na anayetafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasirika)) [Al-'Imraan:85] Na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ametuambia kuwa kutakua na makundi katika ummah wake ambao watawafuata maadui wa Allaah سبحانه وتعالى katika desturi na mila zao kama ifuatavyo: ((ستتبعون سنن من كان قبلكم شبراً بشبر وذراعاً بذراع حتى لو دخلوا جحر ضب لدخلتموه)) قالوا: أتراهم اليهود والنصارى؟ قال: ((فمن إذن؟)) البخاري ومسلم   ((Mtafuata nyendo  za wale waliokuja  kabla yenu  hatua kwa hatua mpaka itafika hadi wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia)) Wa...

NEMBO YETU

Image
Hii ndio nembo yetu tutakayokuwa tunatumia InshaAllah