KUMI LA MWISHO LA MWEZI WA RAMADHANI
Mwenyezi
Mngu Aliyetukuka Ametuwekea ibada tukufu katika kumi la mwisho la
Ramadhani, zenye kuzidisha Imani na kufanya ibada zikamilike na neema
kutimia. Ibada hizi ni Zaka za Fitri na Swala ya Idi. Ametuwekea Zaka za
Fitri ili zimsafishe mwenye kufungana na maneneo machafu na matendo
visivyo faa na ni chakula kwa masikini, na Ametuwekea Swala ya Idi ili
kudhihirisha nguvu za Waislamu na umoja wao na vile wanavyo jikusanya
pamoja.
Ndugu Waislamu, Allah (SW) Anatupenda sana, na
kwa mapenzi yake juu yetu ni kutujalia malipo na thawabu nyingi kwa
kutekeleza ibada ndogo. Mfano Usiku wa cheo ni usiku moja, lakini
thawabu zake ni nyingi kushinda thawabu za ibada katika miezi elfu moja.
Anglia ndugu Muislamu, utukufu na rehma ya Allah juu yetu, lakini wengi
katika Waislmu
hawana khabari na neema kama hizi. Wakati unapita, siku zinapita na
sisi tume ghafilika, mpaka tutakpo fikiwa na mauti ndio tutazunduka na
hali ya kuwa muda umekwisha.
Ndugu
Katika Imani, Khasara kubwa zaidi watapata wale waliofanya bidii
kufunga mwezi huu na kufanya ibada mwanzo wa Mwezi wa Ramadhani, lakini
wanapofikiwa na kumi la mwisho wanarudi nyuma, na kuacha kutekelza ibada
na sunna za Mtume (SAW). Ni khasara ilioje kwa mtu aliefanya bidii
kuchuma mazuri, kisha akashindwa kuendelea na msimamo huo, na kushindwa
kukamilisha kumi la mwisho.
Hukumu ya Ibada ya I’tikaafu:
Ibada
ya I’tikafu ni Suuna. Muislamu anaweza kutekeleza ibada hio wakati
wowote akitaka. Lakini ni Sunna ilio tiliwa mkazo katika Kumi la mwisho
la Mwezi wa Ramadhani. Amesema Aisha: Mtume (SAW) hakuacha katika maisha yake kufanya I’tikaaf katika kumi la mwisho la Mwezi wa Ramadhan.
Mambo yanayo lazimu kufanywa katika I’tikaaf:-
a) Kutia Nia kukaa Msikitini kwa ajili ya kufanya Ibada kwa lengo la kujikurubisha kwa Allah.
b) Kuchagua sehemu ya kukaa katika Msikiti, na kujilazimisha kubaki hapo ila kwa dharura ya kisheria, unaruhusiwa kutoaka.
c) Kujiepusha na tendo la ndoa au njia za kupelekea kufanya tendo hilo.
d) Kufanya
bidii kuzidisha kusoma Qur’an kwa wingi, na kuomba dua kwa wingi.
Kufanya hivyo, itakusaidia kupata usiku wa cheo na kusamehewa madhambi
yako.
e) Kujitahidi kufuata mafundisho ya Mtume katika kutekelez lbada hii.
Mwisho
Ndugu
katika imani, Umri wetu ni mfupi sana, na mwanadamu hajui kama ataweza
kupata nafasi tena kufikia mwezi wa Ramadhani mwakani. Jambo la msingi
ni kufanya bidii na juhudi kubwa kutafuta Usiku wa cheo ili tupate kheri
ya usiku huu. Yule atakaye bahatika kupata usiku huu, kwahakika huyo amefaulu hapa duniani na kesho akhera.
Tunamuomba Allah kwa majina yake matukufu na sifa zake njema atujalie miongoni mwa waja wake Aliyo
wachagua kupata kheri ya Usiku wa cheo. Tunamuomba Allah Atuafikie kwa
kufanya Ibada mbalimbali ambazo anazozipenda na anazoridhia. Tunamuomba
Allah Atuwezeshe kufuata mafundisho ya Mtume Mohammad katika maisha yetu
na atuingize pamoja na yeye katika Jannatul Firdaws.
Comments
Post a Comment