Posts

Showing posts from June, 2014

IBADA YA ITIKAFU.

Image
IBADA YA ITIKAFU. MAANA YA ITIKAFU: Kilugha neno “Itikafu” lina maana kuu mbili, kama zifuatazo: Kuzuia, na Kukaa. Kisheria “Itikafu” ni: Kitendo cha kukaa msikitini kwa mfumo maalumu uambatanao na nia ya kujikurubisha kwa Allah, kwa kutekeleza ibada mbali mbali. HUKUMU YA ITIKAFU: Itikafu ni ibada ya SUNAH katika wakati wo wote na imekokotezwa sana katika kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani. Na itikafu kwa upande mwingine inaweza kuchukua hukumu ya UWAJIBU, hii ni iwapo mtu atajiwajibishia mwenyewe. Mtu atakaposema nimenuia kukaa itikafu siku moja au mbili iwapo nitapata mtoto mathalan. Katika mazingira haya itikafu itakuwa imekwisha kuwa wajibu juu yake. Kwa sababu ya msingi usemao:(Kutekeleza nadhiri ni wajibu). Imepokelewa kwamba Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Mwenye kutia nadhiri ya kumtii Allah, basi na amtii”. Bukhaariy DALILI YA ITIKAFU: Ibada hii ya itikafu imethib...

ISEMAVYO QUR-ANI TUKUFU KUHUSIANA NA SWAUMU YA RAMADHANI SWAUMU YA RAMADHANI KATIKA DIRISHA DOGO. ISEMAVYO QUR-ANI TUKUFU KUHUSIANA NA SWAUMU YA RAMADHANI:

Image
ISEMAVYO QUR-ANI TUKUFU KUHUSIANA NA SWAUMU YA RAMADHANI SWAUMU YA RAMADHANI KATIKA DIRISHA DOGO. ISEMAVYO QUR-ANI TUKUFU KUHUSIANA NA SWAUMU YA RAMADHANI: Allah Mtukufu anasema: “ENYI MLIOAMIMNI! MMELAZIMISHWA KUFUNGA (swaumu) KAMA WALIVYOLAZIMISHWA WALIOKUWA KABLA YENU ILI MPATE KUMCHA ALLAH. SIKU CHACHE TU (kufunga huko). NA ATAKAYEKUWA MGONJWA KATIKA NYINYI AU KATIKA SAFARI (akafungua baadhi ya siku), BASI (atimize) HISABU KATIKA SIKU NYINGINE. NA WALE WASIOWEZA, WATOE FIDIA KWA KUMLISHA MASIKINI. NA ATAKAYEFANYA WEMA KWA RADHI YA NAFSI YAKE, BASI NI BORA KWAKE. NA (huku) KUFUNGA NI BORA KWENU IKIWA MNAJUA. (mwezi huo mlioambiwa kufunga) NI MWEZI WA RAMADHANI AMBAO IMETEREMSHWA KATIKA (mwezi) HUO HII QUR-ANI ILI IWE UWONGOZI KWA WATU, NA HOJA ZILIZO WAZI ZA UWONGOFU NA UPAMBANUZI (wa baina ya haki na batili). ATAKAYEKUWA KATIKA MJI KATIKA HUU MWEZI (wa Ramadhani) AFUNGE. NA MWENYE KUWA MGONJWA AU SAFARINI, BASI (atimize) HISABU (ya siku alizoacha kufunga) KATIKA...

MINBARI YA RAMADHANI

Image
MINBARI YA RAMADHANI Hii ni kutokana na mnasaba wa kuingia mwezi mtukufu wa Ramadhani. Minbari ya Ramadhani itakuwa ikikuletea mawaidha yahusiyanayo na funga ya Ramadhani, ili uweze kuijua funga na hatimaye uweze kufunga kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na kama alivyofunga Bwana Mtume -Rehema na Amani zimshukie – ambaye ndiye kigezo chetu chema. Sambamba na Minbari ya Ramadhani, website yako itakuwa ikikuletea TUNDA LA RAMADHANI. Kupitia tunda la Ramadhani utajifunza hadithi mbili tatu za Mtume zihusianazo na funga tukufu ya Mwezi mtukufu wa ...

RAMADHAN KARIM

Image
RAMADHAN KARIM MAANA YA ‘SAUMU’ Neno ‘Saumu’ ki lugha ya Kiarabu lina maana ya kujizuia. Pia ni neno ambalo lilitumika kabla ya zama za Uislamu. Baadaye Uislamu ulipokuja ukalijaalia neno hili kuwa ni moja kati ya maneno yatumikayo kiibada.Ama maana ya neno hili Kisheria, ni kujizuia kutokana na mambo yanayobatilisha Saumu yaitwayo ‘al-Muftiraat’. Kinyume cha watu wengi wanavyodhani kwamba Saumu hasa ni kujizuia kula na kunywa tu. La Hasha! Bali Saumu ni kukihifadhi kila kiungo chako kutokana na mambo yasiyotakikana. Amesema Imam Ja’far Assadiq, “Kufunga siko kujilinda na kula na kunywa tu, bali utakapofunga hifadhi (chunga) macho yako, ulimi wako, tumbo lako, masikio yako na uchi wako. Vile vile ilinde mikono yako, pendelea sana kunyamaza ila katika heri (tu kama kusoma Qur’ani n.k.) na umhurumie mtumishi wako.” Naye Mtume (s.a.w.) amesema: “Mambo matano hutengua Saumu ya mtu: Uongo, kuseng’enya, kufitinisha, kula viapo vya uongo na (mwanamke) ku mka...

TAHADHARI KUBWA KWA WANAOMILIKI KOMPYUTA,SOMA HII KWA MAKINI

Image
Kitengo cha kimataifa cha kupambana na uhalifu kinawataadharisha watumiaji wote wa kompyuta kuwa wana muda wa wiki mbili kuweza kuhami kompyuta zao dhidi ya mashambulizi ya hali ya juu katika kompyuta hizo. Hili limekuja mara baada ya maafisa wa kimarekani kufanya mkutano na waandishi wa habari wakimtuhumu mwananchi wa nchi ya Urusi kwa kuendesha uhalifu huo unaokadiriwa kufikia Pauni milioni 60. Aina mbili za program mzunguko ambazo ni GOZeuS na CryptoLocker ndio hasa zinazolengwa katika tahadhari hii. Watu wanapewa tahadhari kuhakikisha kwamba program zao za ulinzi (Antivirus) na zile zinazoendesha kompyuta (Operating System) vinakwenda na wakati na  wacheki mara kwa mara iwapo kompyuta zao zipo salama. Taarifa na mafaili muhimu ni vizuri yakawa na njia ya ya nyuma ya kuwezesha kuyapata endapo yatahitajika, kinasema kitengo cah uhalifu cha nchini Uingereza. Programu mzunguko inaharibu kompyuta kwa njia ya viambatanisho au njia mpokeo katika barua pepe. ...