Posts

Showing posts from November, 2011

UTEUZI WA KAMATI MBALIMBALI ZA JUMUIYA YA KCMC MUSLIM ASSOCIATION

KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII 1. OTHMANI WAMALA (MD 3)                                -AMIR 2. SHAMIRU ISMAIL (DIP OPT)                                -KATIBU 3. NYANZA SIMBA  (Bsc. PO)                                    -MJUMBE 4. MARY KAWISHE (AMO)                                        -MJUMBE 5. AMINA MUSHI (...

MWAKA MPYA WA KIISLAM NA HUKUMU YA KUSHEHEREKEA

  Tayari Waislamu tumeingia kwenye mwaka mpya wa Kiislam wa Hijriyah. Sasa ni vipi tuukaribishe mwaka huu wetu mpya? Na nini umuhimu wake kwetu? Na nini hukumu ya kusherehekea? KUHESABIKA MWAKA MPYA Miaka yetu ya Kiislam imeanza kuhesabika baada ya  kuhama (Hijrah)  kwa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  na Maswahaba kutoka Makkah kuhamia Madiynah. Baada ya kuhama, 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhu)   akatoa shauri kuwa kwa vile ni mara ya mwanzo wanahamia katika mji ambao wataanza kutumia sharia’h ya Kiislam, basi ni bora kuanza kuhesabu miaka kwa kuanzia mwezi huo waliohama, nao ni mwezi uliojulikana kama Muharram. Na pia inasemekana kuwa 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhu) alikuwa akipata barua kutoka kwa mabalozi wake wa nchi mbalimbali zilizokuwa chini ya Uislam, na zilikuwa zikiandikwa majina ya miezi bila tarehe. Akawashauri Maswahaba wenzake kuwa kuwe na tarehe. Wako waliopendekeza tarehe zianze kwa kufuata miaka y...

NEEMA ZA PEPO TULIYO AHIDIWA

Maelezo ya Neema za Pepo tuliyoahidiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) yametajwa mno katika Qur-aan na Hadiyth, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): إنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا .   حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا.   وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا. وَكَأْسًا دِهَاقًا. لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا جَزَاء مِّن رَّبِّكَ عَطَاء حِسَابًا.  ((Hakika wenye taqwa [wamchao Allaah] wanastahiki kufuzu. Mabustani na mizabibu. Na wake waliolingana nao. Na bilauri zilizojaa. Hawatosikia humo upuuzi wala uongo. Malipo kutoka kwa Mola wako kipawa cha kutosha)) [An-Nabaa: 31-36] Anasema tena (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Suratul-Waaqiah:  وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ.   أُوْلَئِكَ الْمُقَرَّبُونَ.   فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ.   ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ.   وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ.   عَلَى سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ. مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ.   يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ.   بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَ...

AMKA!!

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (Qiyaama hakitosimama mpaka mitetemeko ya ardhi izidi)   al-Bukhariy Mengi yameandikwa, mengi tumeyasoma, mengi tumeyasikia. Je, haujafika wakati wa kuamka na kuyazingatia yale ya kutusaidia Siku ya Mwisho? Haijawa bado funzo kwetu kama Qiyama kipo chini ya pua zetu kinasubiri amri tu kije kwetu. Dalili ngapi tushaziona? Dalili ngapi tushazishuhudia? Twasubiri hadi milango ya toba ifungwe ndio turudi kwa Mola wetu? SubhaanaAllaah! Ya Sunami hatuyaoni? yaliyowapata watu Duniani, hadi tukawa mashakani, bado tunamuasi Manani? Tumegeuka ashaddu wa kumuasi ar-Rahmaani, hadi kuwa sawa na nyani?  {{ Na bila shaka Tumewaumbia Moto wa Jahannamu wengi katika majini na wanadamu: Nyoyo wanazo, lakini hawafahamu kwazo, na macho wanayo, lakini hawaoni kwayo. Hao ni kama wanyama; hali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walioghafilika. }} [Al-A’araaf: 179] Basi kama ndugu yangu Muislamu unazo nyoyo, fahamu umepewa na macho...

ASALAAM ALEYKUM

Alhamdu lillah rabi ala miin. Shukurani na pongezi ziende kwa Allah muumba wetu na yeye tu ndio mwenye kustahili sifa zote njema. Kulitokea tatizo blog yetu ya kcmcmuslim.blogspot.com ikafungwa kwa hiyo Allah ametuwezesha tumefungua nyingine ambayo inakaribiana sawa na ile kwa jina la www.kcmcmulims.blogspot.com tumeongeza 's' tu kwenye jina la zamani na hii ni kuwajumulisha waislam wa jumuia yoote ya kcmc. Na e-mail yetu ni kcmcmuslims@gmail.com tunaomba mshirikiane nasi hasa kwenye maoni kwenye hii blog na ushauri pamoja na ku-share kwenye facebook na mitandao mingine ya kijamii tutakayokuwa tunayaandika humu. Wabillah tawfiq, Salaaam aleykum.