Posts

Showing posts from 2012

KUMI LA MWISHO LA MWEZI WA RAMADHANI

Mwenyezi Mngu Aliyetukuka Ametuwekea ibada tukufu katika kumi la mwisho la Ramadhani, zenye kuzidisha Imani na kufanya ibada zikamilike na neema kutimia. Ibada hizi ni Zaka za Fitri na Swala ya Idi. Ametuwekea Zaka za Fitri ili zimsafishe mwenye kufungana na maneneo machafu na matendo visivyo faa na ni chakula kwa masikini, na Ametuwekea Swala ya Idi ili kudhihirisha nguvu za Waislamu na umoja wao na vile wanavyo jikusanya pamoja. Lengo la Mada:   Kuwakumbusha watu fadhla za siku kumi za mwisho wa Mwezi wa Ramadhan Kubainisha mafundisho ya Mtume katika siku hizi Kuimarisha mafungamano ya mja na Mola wake, nakufanya bidii kujikurubisha kwa Allah     Utangulizi Enyi Waislamu, Siku za mwezi mtukufu wa Ramadhani zinaendelea kuisha. Na hivi karibuni tutaanza kumi la mwisho. Je ndugu yangu Muislamu umejiuliza suali moja; Je nimefaidika kiasi gani na siku zilizopita? Kuwa mkweli na nafsi yako na u...

HATARI YA KUIHAMA QUR`AN

Image
Anasema Allaah سبحانه وتعالى  (( وَقَالَ الرَّسُولُ يَا رَبِّ إِنَّ قَوْمِي اتَّخَذُوا هَذَا الْقُرْآنَ مَهْجُورًا ) ((Na Mtume amesema: Ee Mola wangu! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur-aan ni kitu kilichohamwa (kilichoachiliwa mbali))) [Al-Furqaan: 30] Allaah سبحانه وتعالى Anatuambia jinsi Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Alivyokuwa akilalamika kuwa watu wake wameihama na kuipuuza hii Qur-aan. Makafiri Quraysh walikuwa hawataki kusikiliza Qur-aan, na ilipokuwa ikisomwa walikuwa wakizungumza upuuzi au kuzungumza kwa sauti za juu mazungumzo mengine ili wasiisikie  kama Anavyosema Allaah سبحانه وتعالى : (( وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لاَ تَسْمَعُوا لِهَذَا الْقُرْآنِ وَالْغَوْا فِيهِ لَعَلَّكُمْ تَغْلِبُون)) ((Na waliokufuru walisema: Msiisikilize Qur-aan hii, na timueni zogo, huenda mkashinda)) [Fusswilat: 26] Hali hii ya kuipuuza Qur-aan vile vile iko miongoni mwa Waislamu hali kadhalika, ingawa Waislamu tofauti yake ni kuwa wameiamini na sio kama Makafiri Q...

Muslim leaders to invite Dr. Bilal Phillips

The chairman of Jamia Mosque Committee Muhammad Osman Warfa said the mindset of many government officials viewed Muslim negatively and it was high time that this culture came to an end. "We should demand the sacking of the director of immigration. He is living on our taxes and Muslims are among the biggest tax payers in the country," he said. Other political leaders who were present included the assistant minister for energy Muhammad Muhamud and nominated MP Muhammad Affey. The meeting was attended by officials from the Supreme Council of Kenya Muslims (SUPKEM), National Muslim Leaders Forum (NAMLEF), Jamia mosque among others. Last week, MPs led by Sheikh Dor and Dujis legislator Adan Duale demanded answers from the Immigration minister on the reason for denying Dr. Bilal Phillips to enter the country. Otieno Kajwang is expected to make his submission to the house next week. The deportation of the Canadian scholar Dr. Bilal Phillips elicited strong condemnation from Muslim l...

MAKATAZO YA KISHARI`AH KWA WANAWAKE

Imekusanywa Na: Abu Faatwimah     Katazo La Kutokuwa Na Shukurani [Kukanusha] Ihsaan Huu dada yangu Muislamu ni uwanja mwingine wenye hatari kubwa, na kwa bahati mbaya ni kuwa wengi miongoni mwa wanawake kwa masikitiko makubwa wameuingia na kuamua kuwa ni katika sehemu zao za kuishi na kutafuta kuridhiwa au kupewa ruhusa ya kwenda watakapo hata kama ni kwenye maasi na pasipo mridhia Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) . Wanawake wengi siku hizi wanapotaka jambo ambalo wanaelewa kuwa mume hatoridhika nalo au halipendi au hata wakati mwingine hayuko tayari nalo kwa sababu moja au nyingine au hata kama hataki ni haki yake; huwa silaha yao kubwa ya kutaka wakubaliwe walitakako kusema usemi wao mashuhuri na wenye kupendeza katika midomo yao: Sikupata kuiona kheri hata siku moja kutokana nawe; yote kwa kuwa amekataliwa siku hiyo alitakalo au amezuiliwa kufanya alitakalo au kwenda atakapo. Mke ni mwepesi wa kusahau au kujisahaul...

SIKUKUU YA WAPENDANAO NA HUKUMU YAKE

Image
BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu was Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa ‘Aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa Ba’ad, Allaah سبحانه وتعالى Ametuchagulia dini ya Kiislamu ambayo ndio dini ya haki na Hatokubali dini yoyote nyingine kama Anavyosema: ((وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الإِسْلاَمِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ))   ((Na anayetafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasirika)) [Al-'Imraan:85] Na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ametuambia kuwa kutakua na makundi katika ummah wake ambao watawafuata maadui wa Allaah سبحانه وتعالى katika desturi na mila zao kama ifuatavyo: ((ستتبعون سنن من كان قبلكم شبراً بشبر وذراعاً بذراع حتى لو دخلوا جحر ضب لدخلتموه)) قالوا: أتراهم اليهود والنصارى؟ قال: ((فمن إذن؟)) البخاري ومسلم   ((Mtafuata nyendo  za wale waliokuja  kabla yenu  hatua kwa hatua mpaka itafika hadi wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia)) Wa...